Skip to content
Home » fataawa Arkanul Islam – Swahili pdf download

fataawa Arkanul Islam – Swahili pdf download

FATAAWA ARKANUL ISLAM - SWAHILI
  • Book Title:
 Fataawa Arkanul Islam
  • Book Author:
Jopo La Wanafunzi, Uthaymin, Yunus Kanuni Ngenda
  • Total Pages
927
  • Book Views:

Loading

  • Click for the  
PDF Direct Download Link
  • Get HardCover  
Click for Hard Copy from Amazon

FATAAWA ARKANUL ISLAM – Sampuli

FATAAWA ARKANUL ISLAM

Swali la 1: Ni nini Tauhidi, na ni vipi vigawanyo vyake?

Jibu: Neno Tauhidi katika lugha ya kiarabu, ni kukifanya kitu kuwa kimoja na hilo haliwezi kukamilika isipokuwa kwa kukataa baadhi ya vitu na kuthibitisha baadhi ya vitu, kwa mfano tunas- ema: haitokamilika Tauhidi ya mtu mpaka kwanza ashuhudie ya kuwa hapana mola apasaye kuabudiwa kwa haki ila Mwenyezi Mungu Mmoja tu, atakapo kuwa amesema maneno haya atakuwa amekataa ya kuwa hakuna Uungu kwa yeyote isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu peke yake.

Na kukataa huku hakumaanishi kuwa hakuna vinavyo abudiwa visivyo kuwa Mwenyezi Mungu hapana, vipo viabudiwa vingine lakini kuabudiwa kwake sio sahihi.

Ni kama unapo sema: Mtu Fulani amesimama maneno haya hayamaanishi kuwa hakuna mwingine aliye simama bali inaweze- kana kuna watu wengine wamesimama pia, lakini unapo sema: Hakusimama yeyote, ina maana hakuna mtu yoyote aliye si- mama, hapa umekataa kusimama kwa yeyote yule na unapo sema: Hakusimama isipokuwa Zaidi hapa unamaanisha hakuna yeyote aliye simama isipokuwa huyu mmoja tu ambaye ni Zaidi, na hii ndiyo Tauhidi, haiwi isipokuwa kwa kukataa vitu na kuthibitisha vitu.

Na Tauhidi  katika  sheria  ya Kiislamu ni: kumpekesha  Mwe-nyezi Mungu  katika yale  mambo  yanayo  muhusu.

Vigawanyo vya Tauhidi.

Wanachuoni wamesema Tauhidi  imegawanyika  ka-tika  sehemu tatu nazo  ni:

1-Tauhidi Rububiyyah (kumpwekesha Mwenyezi Mungu ka-tika umbaji, umiliki na upangaji).

2-Tauhidi  Uluhiyyah  (kumpwekesha  Mwenyezi Mungu katka  ibada). 3-Tauhidi  Asmaa  wa Swifaat (kumpwekesha  Mwenyezi Mungu katika  majina na  sifa  zake).

2-Wanachuoni wamevipata  hivi  vigawanyo  kwa  kuangalia Aya na Hadithi za Mtume rehma na amani ziwe juu yake! Zilizo zungumzia mas’ala ya Tauhidi ndio wakapata ya kuwa imegawa-nyika katika  sehemu  hizo  tatu, na tutaeleza  kila  kigawanyo kwa  urefu  zaidi.

1-Aina ya kwanza ni: Tauhidi Rububuyyah, nayo ni kump-wekesha Mwenyezi Mungu  katka  uumbaji, umiliki  na  upangaji, na  ufafanuzi  wake  ni  kama ifuatanyo;

Katika  kigawanyo  hiki  kuna  vitu  vitatu  muhimu:

1-kuhusu kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika uumbaji wake:

Mwenyezi Mungu  peke yake  ndiye muumba wa kila kitu, hakuna  muumbaji asiyekuwa yeye anasema Mwenyezi Mungu: [Je kuna  muumba mwingine asiyekuwa Mwenyezi Mungu ambaye anapekuni riziki  kutoka katika  mbingu  na  ardhi, hapana Mola mwingine ila Yeye ] [Suratul  Nahli].

Mwenyezi Mungu  peke  yake ndie  muumba, ameumba  kila  kitu  kisha  akakikadiria makadirio yake mpaka vitendo afanyavyo mwanadamu Mwenyezi Mungu ndie aliye viumba kwa ajili hiyo utaona katika  ukamilifu wa kuamini  makadirio ya  Mwenyezi Mungu ni  kuamini  kuwa  Mwenyezi Mungu  ndiye aliyeumba matendo ya waja kama  alivyo sema Mwenyezi Mungu :[Na hali Mwenyezi Mungu ndiye aliye kuumbeni nyinyi na hivyo mna-vyo vifanya!]. [Surat Swaafaati: 96], na hilo ni kwa  kuwa  ma-tendo ya  Mwanadamu ni katika sifa Zake na Mja ni kiumbe wa  Mwenyezi Mungu na mwenye kukiumba kitu ndie muumba wa sifa zake.

Mtu anaweza kuuliza: tutatofautishaje  kati ya uumbaji wa Mwenyezi Mungu  na uumbaji ambao unaweza kutokea kwa asiye  kuwa  Mwenyezi Mungu, kama ilivyo katika maneno yake Mwe-nyezi Mungu:  [Basi ametukuka Mwenyezi Mungu Mbora wa waumbaji.] [Suratul Muuminuna: 14], na maneno yake Mtume rehma na amani ziwe juu yake  kwa wale wenye kupiga  picha: (Kutasemwa kuwaambia vitieni roho vile mlivyo viumba) [Imeipokea Bukhary /2105/na Muslim  /2107/].

Jibu la swali hilo ni kama ifuatavyo:

Asiekuwa Mwenyezi Mungu haumbi kama anavyo umba Mwenyezi Mungu, kwasababa yeye hawezi  kukileta  kitu am-bacho hakipo  na  wala hawezi kumfufua aliye kufa bali uumbaji wa asiye kuwa Mwenyezi Mungu unakuwa ni kukibadilisha kitu kutoka  kwenye sifa fulani kwenda  kwenye sifa nyingine bali ni kile kile kiumbe cha Mwenyezi Mungu  ndio amekibadilisha.

Mfano mtu akipiga picha kitu chochote hakuleta kitu kipya bali atakuwa amebadili kitu  kukipeleka  kwenye kitu kingine, kama vile ambavyo  mtu anaweza kubadili udongo akaufanya kama ndege au akaufanya  kama  picha ya Ngamia.

Na hii  ndio  tofauti  kati ya uumbaji wa Mwenyezi Mungu  na  uumbaji  wa asiye kuwa Mwenyezi Mungu, na kwa ajili hiyo anakuwa Mwenyezi Mungu  ni  mpweke  kwa uumbaji  unaom-husu Yeye  tu.

1-Kumpwekesha  Mwenyezi Mungu  katika  umiliki  wake. Mwenyezi Mungu  peke  yake  ndiye  mmiliki wa  kila kitu kama  alivyo  sema: [Ametukuka yule ambae  katika mikono  yake  kuna ufalme naye kwa kila kitu ni  muweza] [Suratul Mulku] akasema  tena  Mwenyezi Mungu: [Sema ni  nani  mkononi  mwake  umo  Ufalme wa kila kitu ,naye ndiye anaye  linda wala  hakilindwi  asicho  taka,kama  mnajua]  [Suratui  Muuminun].

Mwenye Ufalme wa wafalme wote ni Mwenyezi Mungu peke yake  ufalme ambao  umeenea  katika  kila  kitu na  kunasibisha  ufalme  kwa  asiye kuwa Mwenyezi Mungu ni kunasbisha kwa ziada  tu, na  Mwenyezi Mungu  amethibitisha ufalme  kwa  asiye  kuwa  Yeye  pale  alipo  sema: [Isipo kuwa kwa wake zao au wale walio wamiliki  katika  mikono  yao] [Suratul Muuminun].

Na Aya nyingene nyingi zinazo thibitisha ufalme kwa asiye kwa Mwenyezi Mungu, lakini ufalme huu sio kama ufalme wa Mwenyezi Mungu, kwani ni ufalme ambao una mapungufu na ni ufalme ambao  unamipaka hauenei katika kila kitu, kwa mfano, nyumba anayo imiliki Omar  haimiliki Zaid na nyumba anayo im-iliki Zaidi haimiliki Omar.

Kisha umiliki huu una mipaka, kuwa haruhusiwi mtu kukitu-mia kile anacho kimiliki isipokuwa atumie kama alivyo amrisha Mwenyezi Mungu, utaona kwa ajili hiyo amekataza Mtume rehma na amani ziwe  juu yake! kupoteza mali  hovyo, na amesema Mwe-nyezi Mungu: [Wala  msiwape wasio na akili mali yenu ambayo Mwenyezi Mungu  ameijaalia iwe ni kiamu yenu] [Suratul An Nisaa], na hii ni Ushahidi  ya kuwa umiliki wa mwanadau una ma-pungufu  kisha  ni wenye mipaka, na hii  ni kinyume na Ufalme wa Mwenyezi Mungu kwani ufalme wake ni wenye  kuenea kila kitu usio na mipaka, na Mwenyezi Mungu hufanya  analotaka na wala haulizwi kwa lile analo lifanya, lakini  Mwanadamu  ni mwenye kuulizwa kwa kila anacho kifanya.

3-Kumpwekesha  Mwenyezi Mungu  katika  upangiliaji wake.

Yeye  Mwenyezi Mungu  ndie  anaye pangilia mambo yote ya viumbe  wake  na yeye  ndiye anaye endesha mambo yote katika aridhi  na mbinguni amesema Mwenyezi Mungu: [Fahamuni! Kuumba na  amri zake Ametukuka Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa viumbe nyote]  [Suratul  Araaf].

Na kupangilia huku kumeenea kila kitu hakuna kizuizi wala hakuna mwenya  kupinga  upangaji  wake.

Na kupangilia anako pangilia mwanadamu mambo yake ya kila siku kama kupangilia kuhusu mali zake aziendeshe vipi, na watoto wake awalee vipi na mengineyo, huo ni mpangilio  mfinyu  na  wenye mipaka ni tofauti na mipangilio ya Mwenyezi Mungu ambayo ni mipana  na haina mipaka.

2-Aina ya pili katika aina za Tauhidi ni Tauhiidul Uluuhi-yyah

(Kumpekesha Mwenyezi Mungu katika Ibada)

Nayo ni kumpwekesha Mwenyezi Mungu katika Ibada, mwa-nadamu asiabudu pamoja na Mwenyezi Mungu kitu kingine na asijikurubishe  kwa  kitu  chochote kama  anavyo jikurubisha kwa Mwenyezi Mungu.

Na  aina  hii ya Tauhidi  ndio  ambayo wamepotea  kwayo wen-gi  katika Washirikina  ambao Mtume  Rehma na  amani  ziwe juu  yake! aliwapiga  vita na kuhalalisha damu zao, mali zao, ardhi yao, nyumba zao  na wanawake zao pamoja na watoto wao. Na ndio Tauhidi ambayo Mwenyezi Mungu aliwatuma kwayo Mitume na akashusha Vitabu  pamoja  na Tauhidi Rububuyya na Tauhidi Al-Asmaa wa Swifaat, lakini zaidi walicho kuwa wanakitibu  Mitume  kwa watu  wao  ni Tauhidi  hii, ambayo ni Tauhiidul Uluuhiyyah, ili Mwanadamu asimfanyie Ibada yeyote asiye kuwa Mwenyezi Mungu, awe Malaika au  Mtume au Walii au  Mtu  mwema, au  ki-umbe chochote katika viumbe vya Mwenyezi Mungu, kwasababu Ibada  haiswihi kwa kitu chochote isipokuwa Mwenyezi Mungu.

To read more about the Fataawa Arkanul Islam book Click the download button below to get it for free

or

Report broken link
Support this Website


for websites

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *